Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, nikiambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI nifanye nini?

Je, nikiambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI nifanye nini?

Jambo la msingi ni kutokukata tamaa na kuwa na matumaini. Mara nyingine i inasaidia kama utakuwa ... Read More

Kinga ya mwili ni nini?

Kinga ya mwili ni nini?

Kinga ya mwili ni mpangilio wa mwili kujikinga na maradhi. Chembechembe nyeupe zilizopo katika damu ... Read More
Vidokezo vya Kuwa na Uwazi katika Uhusiano wako na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Uwazi katika Uhusiano wako na Msichana

Kuwa na uwazi katika uhusiano wako na msichana ni jambo muhimu kwa sababu inajenga uaminifu na up... Read More

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Kutoka damu (hedhi) kwa mara ya kwanza kunaitwa kuvunja ungo na hii ni dalili ya mtoto wa kike kuing... Read More
Kwa nini ngozi ya Albino inafanana ya watu weupe?

Kwa nini ngozi ya Albino inafanana ya watu weupe?

Ngozi ya Albino ina ukosefu wa rangi. Inaonekana kama ya watu
weupe ambao wana kiasi cha pig... Read More

Je, unaweza kufa ukitumia dawa za kulevya?

Je, unaweza kufa ukitumia dawa za kulevya?

Ndiyo, unaweza. Kifo kinaweza kuwa cha ghafla au
kutokana na madhara ya muda mrefu katika vi... Read More

Katika tendo la kujamiiana kati ya mwanaume na mwanamke, yupi anayepata starehe zaidi?

Katika tendo la kujamiiana kati ya mwanaume na mwanamke, yupi anayepata starehe zaidi?

Siyo rahisi kusema ni nani anayestarehe zaidi ya mwenziwe, kwa sababu starehe inayotokana na mwan... Read More

Je, mwanaume ambaye ana uwezo wa kumwaga shahawa bila shida, inawezekana kwamba ni mgumba?

Je, mwanaume ambaye ana uwezo wa kumwaga shahawa bila shida, inawezekana kwamba ni mgumba?

Ndiyo, mwanaume ambaye ana uwezo wa kumwaga mbegu bila shida anaweza kuwa mgumba. Kutokuwa mgumba... Read More

Je, kisimi cha mwanamke kikisuguliwa kwa vidole atafikia mshindo? Na kuna madhara yoyote ?

Je, kisimi cha mwanamke kikisuguliwa kwa vidole atafikia mshindo? Na kuna madhara yoyote ?

Ni kweli kwamba kuna sehemu za mwili ambazo zikiguswa huleta msisimko mwilini.

Kisimi (au k... Read More

Je, Ni Vipi naweza kuacha Kufanya Ngono Baada ya Kuanza?

Je, Ni Vipi naweza kuacha Kufanya Ngono Baada ya Kuanza?

Je, Ni Vipi naweza kuacha Kufanya Ngono Baada ya Kuanza?

Jambo la kwanza kabisa, napenda k... Read More

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba

Jinsi ya Kuzungumza na Mwenzi Wako kuhusu Matumizi ya Vidonge vya Kuzuia Mimba 😊

Karibu... Read More

Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Je, mtu anaweza kuambukizwa virusi vya UKIMWI na UKIMWI iwapo atavaliana nguo na mtu mwenye Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Hapana, Virusi vya UKIMWI na UKIMWI hauambukizwi kwa kuvaliana nguo na mgonjwa, kwa sababu vijidu... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About