Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Madhara ya pombe kwa mwili na akili

Featured Image

Pombe huingia kwenye damu na kuzunguka mwili mzima pamoja
na kwenye ubongo wako. Ina madhara kwa viungo vya mwili
wako na ubongo wako na hivyo huathiri tabia na hisia zako.

Unywaji wa pombe kupita kiasi unaweza kuathiri viungo vingi
kwa mfano, ini ambalo ndilo huathirika zaidi. Ini hilo linafanya
kazi ya kufyonza kilevi katika mwili wako. Kama ukinywa zaidi
utaathiri ini kiasi kwamba halitaweza kufanya kazi kikamilifu au
litashindwa kabisa hatimaye utakufa. Kilevi kingi husababisha
kansa ya ini na tumbo.

Hatari kubwa siku hizi ni kupata na kusambaza virusi vya
UKIMWI. Mlevi mara nyingi huwa mzembe na husahau kinga
muhimu kama vile kutumia kondomu wakati wa kufanya mapenzi.
Anaweza pia kufanya mapenzi na watu ambao hafahamu afya
zao, kama ni wagonjwa au la. Zaidi ya hayo mlevi mara nyingi
huwa dhaifu, hivyo ni rahisi kushambuliwa na magonjwa
mbalimbali pamoja na VVU.

Pombe inaathiri pia uwezo wa kufanya tendo la ndoa. Huwa ni
vigumu kwa uume kusimama. Pia huathiri ubongo hasa sehemu
zile zinazomiliki ufahamu na mihemko.

Kwanza unaweza kujisikia mchangamfu na huru, lakini mara
tu unaanza kujisikia taabu na kushindwa kutembea vizuri.
Utakuwa na matatizo ya kutoona vizuri na matatizo ya kutoa
uamuzi sahihi. Watu huanza kuwa na vijitabia vya ajabu na
vipya baada ya kulewa. Kugombana na watu wengine na kufanya
mambo yasiyokubalika kama vile kujikojolea mbele za watu.
Kama utaendelea kunywa kuna uwezekano mkubwa wa kupata
madhara. Kila dhara huharibu mamilioni ya seli za ubongo wa
binadamu.

Kwanza hutakuwa na kumbukumbu ya nini kimetokea, lakini
unaweza pia kupoteza kabisa kumbukumbu zako. Kama ukinywa
pombe kupita kiasi kwa muda mrefu unaweza kupungukiwa
akili na mwisho kuharibu kabisa akili. Pombe pia ni dawa ya
kulevya kwani huweza kukutawala. Watu waliotawaliwa na
pombe, hutumia pesa nyingi na muda mwingi kwenye pombe,
hali ambayo inaweza kuwa ni mzigo mzito kwa familia na jamii,
na pindi mtu anapotawaliwa, ni vigumu kunywa kidogo au kuacha
kabisa. Kama mtu atajaribu kuacha, hupata matatizo kama
kutetemeka, mapigo ya moyo kuongezeka, kutokwa na jasho
jingi, na kukosa usingizi wakati wa usiku. Hali hiyo husababisha
maumivu na ni hatari kwa watu ambao wametawaliwa na pombe.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Nifanyeje Kuelewa umuhimu wa Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI?

Nifanyeje Kuelewa umuhimu wa Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI?

Nifanyeje Kuelewa Umuhimu wa Kujikinga na Maambukizi ya UKIMWI? 🌍

Leo, tutaangazia umuh... Read More

Mapenzi salama ni yapi?

Mapenzi salama ni yapi?

Mapenzi salama ni yale yanayofanyika bila wasiwasi wa kupata mimba zisizotarajiwa, magonjwa ya zi... Read More

Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Ngono na Wazazi?

Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Ngono na Wazazi?

Nifanyeje Kuzungumzia Suala la Ngono na Wazazi? πŸ€”

Karibu kwenye makala hii ambapo tutaj... Read More

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono?

Jinsi ya Kujielewa na Kuelewa Miili Yetu kabla ya Kujihusisha na Ngono 😊😊😊

Karibu... Read More

Je, unaweza kupanga kuzaa aina ya watoto, yaani wa kiume au wa kike tu?

Je, unaweza kupanga kuzaa aina ya watoto, yaani wa kiume au wa kike tu?

Mimba i inatungwa wakati yai la kike linaporutubishwa na mbegu za kiume. Kama tulivyoona hapo juu... Read More

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa ya kujamiiana na ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Je, kuna umuhimu wa kujadili matakwa ya kujamiiana na ngono/kufanya mapenzi katika uhusiano?

Habari wapendwa wasomaji, leo tutaangazia swali muhimu sana ambalo wapenzi wengi hujiuliza. Je, k... Read More

Mimi ni msichana Albino ninaogopa kuwa na rafiki mwanaume kwa kuhofia kuwa anataka tu kujamiiana na mimi na halafu aniache

Mimi ni msichana Albino ninaogopa kuwa na rafiki mwanaume kwa kuhofia kuwa anataka tu kujamiiana na mimi na halafu aniache

Wakati mwingine kuwa na muonekano tofauti na watu wengine
huvuta udadisi. Na hasa tukikumbuk... Read More

Je, nifanye nini ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Je, nifanye nini ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Hakuna chanjo dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI, Lakini kuna mienendo ya tabia a... Read More

Je, ni lazima kumeza vidonge vya kuzuia mimba siku zote, hata zile siku nisipojamiiana?

Je, ni lazima kumeza vidonge vya kuzuia mimba siku zote, hata zile siku nisipojamiiana?

Ndiyo, vidonge vya kuzuia mimba ni lazima vimezwe kila siku hata kama hufanyi ngono siku hiyo. Ku... Read More

Kwa nini kuna Watanzania wanaovuta bangi?

Kwa nini kuna Watanzania wanaovuta bangi?

Sababu mojawapo ni kuwa bangi hulimwa hapa nchini na
hivyo hupatikana kwa urahisi. Bangi huu... Read More

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Thamani yangu katika Mahusiano ya Ngono?

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Thamani yangu katika Mahusiano ya Ngono?

Nifanyeje Kujielewa na Kuelewa Thamani yangu katika Mahusiano ya Ngono? 🌟

Asante kwa ku... Read More

Jinsi ya Kujenga Uaminifu katika Uhusiano wako na Msichana

Jinsi ya Kujenga Uaminifu katika Uhusiano wako na Msichana

Jinsi ya Kujenga Uaminifu katika Uhusiano wako na Msichana

Katika uhusiano wowote, uaminif... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About