Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Wosia mzuri wa baba kwa mwanae

Featured Image

Mwanangu, mimi baba yako nimeishi miaka mingi kuliko wewe ndio maana unaniita baba. Ni kweli sijasoma kama wewe ulivyosoma Ila mambo niliyokutana nayo tangu nimezaliwa ni elimu tosha ambayo wewe huna. Sasa nataka nikupe Elimu hiyo ili ukijumlisha na elimu yako ya darasani ujue namna nzuri ya kuishi katika dunia hii iliyojaa mishangazo mingi.

Maisha ni jumla ya mambo yote unayoyatenda kila siku. Namaanisha kila unalolifanya Leo linaathiri maisha yako ya kesho kwa hali chanya au hali hasi. Na kama ni hali hasi ni kwa ukubwa gani halikadharika kama ni hali chanya ni kwa kiwango gani. Mwanangu kila jambo unalolifanya Leo huamua ni mlango gani Unaweza ingia Kesho lakini pia mlango upi huwezi ingia Kesho. Ndio maana ni muhimu kuijua Kesho yako ukiwa Leo.

Mwanangu ili ufanikiwe ni lazima ujue kuishi na watu vizuri. Na mimi sikushauri kabisa kwamba uwe na marafiki wengi. Kuwa na marafiki wengi ni moja ya eneo unaweza jitengenezea mtego mbaya wa kukuangamiza kesho yako. Mwenye hekima mmoja aliwahi kusema ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe. Mwanangu kwa kusema hivyo simaanishi uwe na maadui,hapana. Ila marafiki zako watakusaidia mlango unaotaka kuingia Kesho uingie kwa urahisi au kwa ugumu au usiingie kabisa na wakati mwingine Unaweza kuingia na wakahusika kukutoa kwa aibu kubwa. Ndio maana ni muhimu Kuwa na marafiki ila Kuwa nao wachache chagua kwa makini mno. Sio lazima kila akufaaye kwa dhiki ndiye awe rafiki. Kuna watu wanakufaa kwa dhiki Leo ila Kesho wakutumikishe Kuwa makini sana.

Mwanangu, kuwa makini sana na mahusiano yako ya kimapenzi maana yanagusa hisia zako na mtu unayehusiana naye moja kwa moja. Hivyo basi kuwa makini maana mahusiano hayo yanaweza kukufanya Kesho ukamkosesha raha utakayekuwa naye kama sio huyo uliyenaye leo ndie ukajaaliwa Kuwa naye Kesho. Mwanangu, Unaweza kuniona mshamba sababu ulimwengu wenu unaonekana kama haujali sana haya mambo ila tafadhari zingatia utakapofika Kesho utaelewa sana hiki ninachokuambia.

Mwanangu, jichunge sana na mambo unayoyafanya Leo na uwe muungwana na kupenda haki. Tamaa isikupeleke ukafanya mambo mabaya ambayo yatakulazimisha kutunza siri moyoni mwako hata kama utafika ile Kesho yako. Jiepushe kabisa na mambo mabaya ya siri ya nafsi. Hakuna utumwa mbaya kama utumwa ndani ya nafsi yako mwenyewe maana kila ukikumbuka nafsi itakusuta na kukukosesha raha ya kweli. Hivyo kubali na kuridhika na ulivyo kama huwezi kujiongeza kwa njia halali na za haki. Ni heri uwe masikini mwenye uhuru ndani kuliko uwe tajiri na maarufu mwenye siri mbaya ndani ya Moyo wako. Mwanangu tafadhari uwe makini sana.

Mwanangu, siwezi sahau kukwambia kuhusu Mungu. Maisha ya uchaji wa Mungu yatakuepusha na mengi. Hapa naomba unielewe kwamba usijifanye unamcha Mungu bali mche Mungu. Sio kwasababu unashida ya kufanikiwa ndio umche Mungu, hapana! Bali umche Mungu sababu ni Mungu na yeye ndiye anaijua Kesho yako vizuri kuliko wewe mwenyewe. Ukimshirikisha mambo yako na ukawa mwaminifu kwake hakika hatakuacha kamwe.

Mwanangu, usiku umeenda nenda kalale sasa ila usije ukapenda na kutamani waovu kwa uovu wao na wakakushawishi ujiunge nao. Tafadhari usikubali.

#Kizazi Ganzi#

JIFUNZE KUJIFUNZA

Mwl Makwaya
Kuwa Ni Kufanya.

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki niย Soft copy [pdf]ย kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

[products columns="2" ids="30827"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kudumisha afya na ustawi wa akili

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kudumisha afya na ustawi wa akili

Kusaidiana na mpenzi wako katika kudumisha afya na ustawi wa akili ni muhimu katika kujenga uhusiano... Read More
Njia za Kuimarisha Ushirikiano na Kujenga Ushawishi katika Mahusiano yako

Njia za Kuimarisha Ushirikiano na Kujenga Ushawishi katika Mahusiano yako

Leo, tutajadili juu ya njia za kuimarisha ushirikiano na kujenga ushawishi katika mahusiano yako.... Read More

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Vidokezo vya Kuwa na Mazungumzo ya Kina na Msichana

Kama kijana, kuna wakati unaweza kukutana na msichana na unataka kuzungumza naye kwa kina lakini ... Read More

Kukabiliana na Changamoto za Mahusiano: Mazoea Bora na Mbinu

Kukabiliana na Changamoto za Mahusiano: Mazoea Bora na Mbinu

Kukabiliana na Changamoto za Mahusiano: Mazoea Bora na Mbinu

Mahusiano ni sehemu muhimu sa... Read More

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kutokuelewana na Kukosa Msamaha katika Familia Yako

Njia za Kupunguza Mazoea ya Kutokuelewana na Kukosa Msamaha katika Familia Yako

Familia ni nguzo muhimu sana katika maisha yetu na tunapaswa kuilinda kwa gharama yoyote ile. Hat... Read More

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiuchumi na mpenzi wako

Jinsi ya Kuelewa na kushughulikia tofauti za kiuchumi na mpenzi wako

Kwenye uhusiano wowote, tofauti zinajitokeza kwa sababu kila mtu ana mawazo yake na maoni yake to... Read More

Ishara 10 za mwanamke aliyekuzimia na anayekupanda

Ishara 10 za mwanamke aliyekuzimia na anayekupanda

Ishara hizi zinaweza zikakusaidia kumgundua msichana anayekupenda, wasichana wanatofautiana ila w... Read More

Kujenga Mazoea ya Kuheshimiana na Kuthamini maoni ya Kila Mwanafamilia katika Familia Yako

Kujenga Mazoea ya Kuheshimiana na Kuthamini maoni ya Kila Mwanafamilia katika Familia Yako

Kujenga Mazoea ya Kuheshimiana na Kuthamini maoni ya Kila Mwanafamilia katika Familia Yako

Read More
Jinsi ya Kusimamia Mipaka na Kanuni katika Familia: Kuwa na Muongozo

Jinsi ya Kusimamia Mipaka na Kanuni katika Familia: Kuwa na Muongozo

Kusimamia mipaka na kanuni katika familia ni muhimu sana kwa ustawi wa familia yako. Ili kuwa na ... Read More

Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke

Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke

Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke au Hatua za kufuata kuamsha hisia za mwanamke ... Read More

Njia za Kusuluhisha Tofauti za Maoni katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kusuluhisha Tofauti za Maoni katika Uhusiano wako na Msichana

Hakuna jambo gumu kama kusuluhisha tofauti za maoni katika uhusiano wako na msichana wako. Wakati... Read More

Jinsi ya Kuimarisha Upendo na Kuunda Maisha ya Ndoa yenye Maana na mke wako

Jinsi ya Kuimarisha Upendo na Kuunda Maisha ya Ndoa yenye Maana na mke wako

Kuimarisha upendo na kuunda maisha ya ndoa yenye maana na mke wako ni muhimu katika kudumisha uhusia... Read More
๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About