Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

Ushauri kwa vijana wenye miaka 22 nakuendelea

Featured Image

Ikiwa wewe ni kijana na Una umri wa kuanzia miaka 22 na Kuendelea
Soma hapa ujifunze maisha ya hekima na namna bora ya kuishi na kufanikiwa ungali kijana

1. Kama uko shule au chuo soma na usicheze ukifeli unajipotezea muda. Soma sana utafanikiwa…

2. Jifunze kuweka akiba ya pesa. Pia jifunze kuwa na matumizi mazuri ya pesa,bajeti vizuri na jiwekee akiba bank au popte unapoona panafaa.

3. Jitengenezee good character yaani tabia yako njema ili uwe tofauti na wengine.. Jitofautishe na wengine, uwe mfano bora

4. Jifunze kufanya kazi tofauti tofauti. Fanya hiki ama kile ili angalau uweze kuishi popote kwani dunia inabadilikaa na huwezi jua kesho yako

5. Anza kununua na kumiliki vitu kama kitanda godoro vyombo na ardhi au kiwanja. Kumbuka msingi mzuri wa maisha ni fikra za ujana na kujiwekea mali

6. Kama utaweza kapange ujifunze maisha. Anza kujitegemea ili kujipa confidenece na maisha.

7. Weka falsafa yako katika maisha na uiishi. Falsafa ni dira ya kukuongoza. Mfano unataka kumiliki nini katika maisha? Unataka mke au mume wa aina gani? Aina gani ya maisha unaipenda? Hiyo ndiyo falsafa…

8. Tengeneza mahusiano yaliyotulia na weka malengo. (Kwa wale wa ndoa) Jichagulie kijana au binti aliyemzuri katika wengi, kijana au binti wa moyo wako, mpende… Kipindi hiki ni cha kuwa na mwenza aliyetulia kama unafikiri kuoa au kuolewa. Ukicheza ukafikisha 30 bila kuwa na mtu maaalumu basi utaoa au kuolewa bora mradi ila siyo na mtu wa ndoto yako..

9. Kuwa na marafiki imara, jichagulie katika wengi marafiki kadhaa waliotulia wenye nidhamu ya maisha na wanaopenda uende mbele. Kijana chunga marafiki ulionao wengi leo wanajuta kwaa urafiki m'baya uliowapoteza… a

10. Kumbuka ibada na kumshukuru Mungu. Kipindi hiki ni cha misukosuko na mihemko mingi. Usiache mafundisho ya imani yako, usimsahau Mungu. Mshukuru Mungu kwa uhai na kila jema au baya likupatalo.

11. Jitume katika kazi, watu waliofanikiwa wanajua thamani ya juhudi na kujituma. Usikate tamaa hata kama unapata kidogo. Fanya kazi kama vile kesho haipo. Matunda utayaona

12. Zingatia kujiweka safi. Kuwa msafi na mtanashati huanza na ubongo, muonekano wako ndivyo watu watakavyo kuchukulia. Jiweke safi na jitunze..

13. Kula kwa afya, wengi wanachukia miili yao. Wanauchukia aidha unene au wembamba, ila ukila kwa afya, ukafanya mazoezi unatengeneza afya bora ya sasa na baaadae..

14. Vaa kwa heshima, usivae kama mcheza disko au teja. Kumbuka thamani yako kwa Mungu. Kwanini uvae nguo za machukizo mbele yake! Kwanini ukubali kuwa wakala na kutumiwa na shetani kuwaaangamiza wengine kwa kuvaa ovyo? Vaa kwa heshima..

15. Pendelea kusafiri maeneo tofauti na ujifunze! Asafiriye hupata maarifa na hujifunza mengi. Penda kusafiri, tembelea maeneo tofauti utakuwa na mengi ya kujifunza.

16. Kumbuka kupumzisha mwili. Kuishi kwetu kupo katika chembe ya uhai iliyopo mwilini. Upe mwili na ubongo chakula chake cha kupumzika. Nenda maeneo yatakayofanya mwili na akili vipumzike angalau kila baada ya miezi kadhaa..

17. Jifunze kuamua mwenyewe. Usisubiri kila kitu kumshirikisha mtu ndio uamue. Jifunze kuwa mwamuzi wa mambo yako mwenyewe haijalishi kwa gharama ipi. Watu wawe washauri ila ubaki kuwa mwamuzi mwenyewe.

18. Kuwa mtu wa kutunza siri. Jitahidi kuwa na shingo nzito na akili yenye kuweka siri. Usiwe mtu wa kusema kila uonacho au uambiwacho.

19. Jfunze na zitawale hisia zako. Hisia ziwe za hasira, mapenzi au ugomovi zitawale na utaishi miaka mingi. Asiye tawala hisia zake hata awe mkubwa bado ni mdogo…

20. Jitolee kwaajili ya wengine, fundisha kemea saidia. Unaweza kufundisha kupitia facebook wasap nk. Kemea ukiona mtu anafanya kitu kibaya, saidia wenye shida wakumbuke wagonjwa yatima wazee na wenye mahitaji. Wewe ni yatima, mzee, au muhitaji wa kesho.. Weka akiba ya wema

21 Jenga mazingira ya kuishi na watu vizuri. Usijione mzuri au HB sana ukadharau wengine. Ishi na kila mtu kwa upendo hata kama wanakuchukia..

22. Tunza muda, muda ni mali huwezi kuurudisha, kuusimamisha au kuuzuia. Ukishapotea ndio basi tena. Tambua thamani ya muda na fanya vitu kwa wakati..

23. Pendelea kusoma hasa vitabu vya dini, kuhusu mali, elimu, mchumba, afya, maisha, uongozi, hekima, busara, utu, uchaji, utii, maarifa, utajiri, heshima, uvumilivu, matumaini, upendo, na kila kitu vimo katika Biblia na Qur'an ..soma uchote hekimaa…

24. Acha kujifunza matumizi ya pombe, sigara , dawa za kulevya. Kama unatumia jitahidi uache, kama unajifunza acha na kama kuna mtu anakushawishi kataa. Afya ni mali na mtaji usichoshe na kuumiza uhai wako kwa pombe sigara na madawa ya kulevya…

Inafaa ukishare kwa wengine wajifunze maarifa haya..
*Maisha ni maamuzi yako wewe*
Kuamua kufanikiwa au kushindwa,
kuamua utajiri au umasikini yote ni mipango na hutokana na fikra zako..

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Mshikamano katika Familia: Kuunda Nafasi ya Kusaidiana

Kukabiliana na Mazoea ya Kukosa Mshikamano katika Familia: Kuunda Nafasi ya Kusaidiana

  1. Familia ni sehemu muhimu sana katika maisha yetu, lakini mara nyingi mazoea ya kukosa m... Read More

Kuhamasisha Furaha na Uchangamfu katika Familia Yako

Kuhamasisha Furaha na Uchangamfu katika Familia Yako

Kuhamasisha Furaha na Uchangamfu katika Familia Yako

Familia nzuri ni ile ambayo inajumuis... Read More

Je, katika kujaribu fantasia za ngono/kufanya mapenzi pamoja na mwenza wako?

Je, katika kujaribu fantasia za ngono/kufanya mapenzi pamoja na mwenza wako?

Je, katika kujaribu fantasia za ngono/kufanya mapenzi pamoja na mwenza wako? Hii ni mada ambayo i... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujifunza na kukuza katika uhusiano

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujifunza na kukuza katika uhusiano

Kusaidiana na mpenzi wako katika kujifunza na kukua katika uhusiano ni muhimu kwa maendeleo yenu bin... Read More
Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu matatizo ya kiuchumi na madeni

Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu matatizo ya kiuchumi na madeni

Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu matatizo ya kiuchumi na madeni ni muhimu katika kujenga uelewa na k... Read More
Je, kuwa kuna mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhusu ngono/kufanya mapenzi?

Je, kuwa kuna mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhusu ngono/kufanya mapenzi?

Habari yako, mpenzi! Katika mada ya leo, tunajadili kuhusu mambo ambayo hayafai kuzungumziwa kuhu... Read More

Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mipango ya elimu na ukuaji binafsi

Jinsi ya Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mipango ya elimu na ukuaji binafsi

Kuzungumza na mpenzi wako kuhusu mipango ya elimu na ukuaji binafsi ni njia nzuri ya kuendeleza na k... Read More
Kujenga Ushirikiano wenye Kusaidiana na Kuwa na Amani na Furaha katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Kusaidiana na Kuwa na Amani na Furaha katika Familia

Kujenga Ushirikiano wenye Kusaidiana na Kuwa na Amani na Furaha katika Familia

Familia ni ... Read More

Njia za Kudumisha Mapenzi katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kudumisha Mapenzi katika Uhusiano wako na Msichana

Mapenzi ni muhimu katika uhusiano wowote wa kimapenzi. Ni muhimu kuchukua hatua za kudumisha mape... Read More

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha uhusiano mzuri na wazazi wenu

Jinsi ya Kusaidiana na mpenzi wako katika kujenga na kudumisha uhusiano mzuri na wazazi wenu

Uhusiano mzuri na wazazi wako ni muhimu sana katika kudumisha furaha na amani katika familia. Kwa... Read More

Kuelewa na Kuheshimu Aina tofauti za Ushawishi wa Kufanya Mapenzi: Ujinsia kama Wigo

Kuelewa na Kuheshimu Aina tofauti za Ushawishi wa Kufanya Mapenzi: Ujinsia kama Wigo

Kuelewa na Kuheshimu Aina tofauti za Ushawishi wa Kufanya Mapenzi: Ujinsia kama Wigo

Kufan... Read More

Kuvunja Vizuizi vya Aibu katika Kufanya Mapenzi: Njia za Kuweka Urahisi na Utulivu

Kuvunja Vizuizi vya Aibu katika Kufanya Mapenzi: Njia za Kuweka Urahisi na Utulivu

Kuvunja Vizuizi vya Aibu katika Kufanya Mapenzi: Njia za Kuweka Urahisi na Utulivu

Kufanya... Read More

📖 Explore More Articles
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About