Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE 🔁
AckyShine

Ujumbe kwako wewe mwajiriwa au uliyejiari

Featured Image

Kama umeajiriwa au pia umejiajiri ni mojawapo ya njia zinazokuingizia kipato maana wengi wanaanzia hapo mpaka kuja kufikia kule wanakohitaji.
Ila kuna maswali machache ya kukupa changamoto ambayo nataka ujiulize:-

Kwako muajiriwa

👉🏿Umeshawahi kujiuliza huo mshahara unaolipwa unakutosha kukutimizia Yale yote unayohitaji maishani mwako??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ukifukuzwa au ukipunguzwa kazini utafanya nini?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ofisi au kampuni unayofanyia ikifilisika wewe utafanya nini?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka kuhama au kuacha kazi hapo unapofanyia uende ofisi nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwanini hupapendi hapo unapoishi lakini bado unaendelea kuishi hapo?

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini huo usafiri unaoutumia huupendi lakini kila siku unautumia huo huo??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza ni kwa nini wanao au watoto wako hawapendi shule wanayosoma lakini wewe uwezo wako ndipo ulipoishia??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini hupendi mikopo lakini bado unaendelea tu kukopa??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza unaipenda kwa dhati tena kutoka moyoni kazi unayoifanya??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unaomba kila Mara kuongezewa mshahara kama sio kuandamana??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unatamani ukasome uongeze elimu??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini mkubwa wako kazini hataki uache kazi au ukasome au uhamie ofisi nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini kila siku uko "busy" kazini au ofisini mpaka unakosa muda wa kufurahia na ndugu,jamaa,na marafiki na familia na mifuko yako au akaunti yako benki haiko "busy"??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka kufungua kibiashara chako au unataka ufanye kilimo Fulani kwa sababu umesikia kinawatoa watu???

👉🏿Umeshawahi kujiuliza usipokwenda kazini kwa muda Wa wiki au mwezi au mwaka je kipato hicho hicho unachokipata utaendelea kukipata??

Hebu jiulize hayo maswali na mengine mengi yanayofanania na haya ujaribu kuona kama majibu yake unayo na kama majibu yapo ni njia gani unatumia au unategemea kutumia ili kuondokana na hayo??

Kwako wewe uliyejiajiri

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini biashara yako haikui kwa muda wote huo uko pale pale??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini unataka uachane na hiyo biashara ufanye nyingine??

👉🏿Umeshawahi kujiuliza kwa nini kila kitu unafanya wewe mwenyewe haumruhusu msaidizi kuwepo??

👉🏿Kwa nini huthubutu kumuachia mtu biashara yako kwa muda tu ukiondoka unafunga??

👉🏿Kwa nini unawaumiza wengine au wengine wanaumia ndipo wewe utengeneze faida yako??

👉🏿Kwa nini huwezi kuwasaidia wengine waweze kutengeneza kipato kama chako??

👉🏿Kwa nini akija mwenzako pembeni yako kufungua biashara kama yako unachukia???

👉🏿Kwa nini unachukia kulipa kodi ya pango lakini inakubidi tu ufanye hivyo??

👉🏿Ni watu wangapi wanaichukia au kuipenda biashara yako??

👉🏿Wangapi wanakuongea vizuri au vibaya kutokana na Huduma yako unayotoa??

👉🏿Kwa nini unatamani usiwe unalipa kodi??

👉🏿Kwa nini hupendi kuwaonyesha wengine njia unazotumia katika kuijenga biashara yako??ikiwa ni pamoja na upatikanaji Wa mizigo,unavyouza na unavyopata Wateja??kwa nini?

👉🏿Kwa nini hupendi kuona aliyeanza nyuma yako akifanikiwa kabla yako??

Hayo ni baadhi ya maswali ya kujiuliza wewe kama mjasiriamali au uliyejiajiri ingawa yapo na mengine unaweza kujiuliza tu uone kama utapata majibu yake na yawe ya kueleweka

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Tabia za kuepuka ili uweze kuwa tajiri

Tabia za kuepuka ili uweze kuwa tajiri

UKIWA NA HIZI TABIA 9, JIANDAE KUFA MASKINI…………
By Kashindi EdsonRead More

Jielewe, kipato chako kinakusaidia nini?

Jielewe, kipato chako kinakusaidia nini?

ASSET AND LIABILITY
Asset ni kitu... Read More

Mizigo tuliyoibeba ambayo haina faida

Mizigo tuliyoibeba ambayo haina faida

1.💥Umejipa jukumu la kuwa "mpelelezi" wa maisha ya wengine na umesahau maisha yako.

2.... Read More

Jipe moyo kamwe usikate tamaa

Jipe moyo kamwe usikate tamaa

Nilikuwa naangalia mpira wa miguu katika uwanja wa
shule.
Nilipokaa, Nilimuuliza kijana... Read More

Siri za mafanikio na Jinsi ya kufanikiwa

Siri za mafanikio na Jinsi ya kufanikiwa

Tafuta fursa kila kona.
Tumia kipaji chako.
Kuwa na nidhamu katika fed... Read More

Salamu za kuaga mwaka na kukaribisha mwaka mpya

Salamu za kuaga mwaka na kukaribisha mwaka mpya

KWAHERI MWAKA JANA. UMENIFUNZA MENGI.

Mwaka umefika mwisho, zimebaki siku tatu tu
kuin... Read More

Kukataliwa ni mtaji

Kukataliwa ni mtaji

Hakuna mtu duniani ambaye hajawahi kukutana na hali ya kukataliwa. Yaani kukataliwa katika hali y... Read More

Wewe ni mshindi: Mambo yakuzingatia ili uweze kushinda chochote katika maisha

Wewe ni mshindi: Mambo yakuzingatia ili uweze kushinda chochote katika maisha

Mshindi ni mtu aliyeshinda, Hivyo wewe ni mshindi kwa kuwa umeshinda, kuwa hai leo ni ushindi, ku... Read More

Elimu ya biashara

Elimu ya biashara

Jifunze kujikagua, jifunze kujiuliza je hapa ndipo napotakiwa kuwa? Usifurahie tu kwamba upo hapo... Read More

AMINI UNA AKILI YENYE UWEZO MKUBWA WA KUBUNI WAZO LA KUWEZA KUKUSAIDIA KUFANIKIWA KIMAISHA

AMINI UNA AKILI YENYE UWEZO MKUBWA WA KUBUNI WAZO LA KUWEZA KUKUSAIDIA KUFANIKIWA KIMAISHA

AMINI UNA AKILI YENYE UWEZO MKUBWA WA KUBUNI WAZO LA KUWEZA KUKUSAIDIA KUFANIKIWA KIMAISHA.

Read More
Ujumbe kwa leo

Ujumbe kwa leo

Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika…Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia…Kuna HELA huwezi kuzipata... Read More

Jifunze kupitia mfano huu Ili uishi kwa amani na watu

Jifunze kupitia mfano huu Ili uishi kwa amani na watu

Siku moja nilichukua taxi aina ya UBER nikiwa naelekea uwanja wa Ndege Mwl. Nyerere Dereva huku a... Read More

📖 Explore More Articles
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About