Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Magonjwa ya zinaa na dalili zake

Featured Image
Kuna magonjwa mengi tofauti ya zinaa, lakini yale ambayo yameenea sana ni kisonono, kaswende, klamdia, kankroidi, utando mweupe , Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Shida kubwa ya magonjwa mengi ya zinaa ni kwamba dalili zake hazionekani kwa urahisi na kama yasipotibiwa kikamilifu yanaweza kuleta madhara makubwa. Maelezo kuhusu magonjwa ya zinaa yaliyoenea sana ni kama yafuatayo:

Kisonono:

Huchukua muda wa siku 1 hadi 14 tangu kuambukizwa mpaka kuonyesha dalili za kuumwa. Kwa wanawake dalili za kisonono ni maumivu chini ya tumbo ambayo yanaweza kuambatana na homa na kutokwa uchafu ukeni. Wapo wanawake wengine ambao hawaoni dalili zozote. Kwa wanaume dalili ni kutokwa na usaha uumeni na kupata maumivu wakati wa kukojoa. Athari yake kwa mwanamke ni kuziba mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi, na vilevile ugumba. Kwa mtoto aliye tumboni mwa mama mjamzito kisonono cha mama yake kinaweza kusababisha upofu. Kwa mwanaume athari yake ni kuziba mirija ya kupitisha mkojo.
The ListPages module does not work recursively.

Kaswende:

Dalili ya kaswende kwa mwanamke ni vidonda sehemu za siri hasa kwenye mashavu ya uke na sehemu ya njia ya haja kubwa, pamoja na sundosundo sehemu ya siri. Kwa mwanaume dalili ni vidonda. Mara nyingi kimoja kwenye kichwa cha uume, kwenye kishina cha uume na kuzunguka njia ya haja kubwa. Pia mwanaume anaweza kupata sundosundo sehemu za siri. Ugonjwa huu husababisha matatizo ya moyo, na kuharibu ubongo na kuzaa watoto walemavu.

Klamdia:

Dalili yake kwa mwanamke mara nyingi siyo rahisi kuonekana. Kwa mwanaume dalili ni kupata maumivu wakati wa kukojoa, na kukojoa mara kwa mara. Athari kwa mwanamke ni kuziba kwa mirija ya kupitisha mayai na mimba kutunga nje ya mfuko wa uzazi. Mimba hizi kuhatarisha maisha ya mama na kuleta ugumba vinaweza kutokea. Kwa mwanaume athari ni kuziba mirija ya kupitisha mbegu na utasa.
The ListPages module does not work recursively.

Kankroidi:

Dalili yake ni vidonda sehemu za siri vinavyokuwa na maumivu makali, maumivu wakati mkojo unapopita kwenye vidonda na kuvimba tezi sehemu za siri. Tezi huweza kupasuka na kutoa uchafu na maumivu makali.

Utando mweupe:

Dalili kwa mwanamke ni kutokwa na uchafu ukeni (kama maziwa yaliyoganda), kuwashwa na kuwa na michubuko sehemu za siri. Kwa mwanaume ni kuwashwa sehemu za siri na kusikia maumivu wakati wa kukojoa. Athari ni maumivu wakati wa kujamiiana.
The ListPages module does not work recursively.

Virusi vya UKIMWI:

Katika hatua ya mwanzo baada ya kuambukizwa hakuna dalili maalum. Hatua hii inaweza kuchukua mpaka miaka kumi. Lakini mara mtu anapoanza kuugua UKIMWI dalili zinakuwa nyingi. Pamoja na kupungua kinga ya mwili, kupungua uzito na kuumwa mara kwa mara. Matokeo ya kuugua UKIMWI baada ya muda fulani ni kifo.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Siku ya Kumbukumbu ya Kipekee na Msichana

Kumbukumbu zetu ni muhimu sana katika maisha yetu. Siku ya kumbukumbu ni siku muhimu sana kwa sab... Read More

Kwa nini Albino tunaonekana kama mzigo katika familia zetu?

Kwa nini Albino tunaonekana kama mzigo katika familia zetu?

Watu wanaohitaji kupewa uangalizi maalumu wanaweza
kuonekana ni mzigo kwa kuwa wanaweza waka... Read More

Sheria kuhusu kufanya punyeto

Sheria kuhusu kufanya punyeto

Punyeto ni kupapasa au kusugua kiungo cha uzazi ili uweze kupata
starehe. Hakuna kosa kwa te... Read More

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Kwa nini wasichana wakiingia utu uzima damu zinaanza kutoka kwenye uke?

Kutoka damu (hedhi) kwa mara ya kwanza kunaitwa kuvunja ungo na hii ni dalili ya mtoto wa kike kuing... Read More
Njia za Kusuluhisha Migogoro katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kusuluhisha Migogoro katika Uhusiano wako na Msichana

Wakati mwingine, migogoro katika uhusiano wako na msichana inaweza kuonekana kama jambo lisilowez... Read More

Je, inafaa kuzungumzia kuhusu historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano?

Je, inafaa kuzungumzia kuhusu historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano?

Je, kuna haja ya kuzungumzia historia ya ngono/kufanya mapenzi ya kila mmoja katika uhusiano? Jib... Read More

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Njia za Kujenga Hisia za Usalama katika Uhusiano wako na Msichana

Hakuna kitu kizuri kama ... Read More

Ni asilimia ipi ya Watanzani ambao wameambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Ni asilimia ipi ya Watanzani ambao wameambukizwa na Virusi vya UKIMWI na UKIMWI?

Nchini Tanzania ni 7% ya watu wenye umri kati ya miaka 15-49 wana maambukizi ya Virusi vya UKIMWI... Read More

Je, Tanzania kuna Albino wangapi?

Je, Tanzania kuna Albino wangapi?

Idadi kamili ya Albino Tanzania haijulikani kwani hakuna
aliyewahesabu. Inakisiwa kufuatana ... Read More

Ninaweza kupata mimba wakati nipo kwenye hedhi?

Ninaweza kupata mimba wakati nipo kwenye hedhi?

Ili mwanamke aweze kushika mimba, i inabidi yai lililopevuka likutane na mbegu za kiume. Yai pevu... Read More

Jeshi la polisi linafanya nini katika kukomesha mauaji na madhara yanayotendeka kwa Albino?

Jeshi la polisi linafanya nini katika kukomesha mauaji na madhara yanayotendeka kwa Albino?

Jeshi la polisi limeanza mikakati maalumu kuchunguza masuala
yote yanayohusu vitendo hivyo, ... Read More

Ugumba wa mwanaume unasababishwa na nini?

Ugumba wa mwanaume unasababishwa na nini?

Ugumba wa mwanaume ni hali ya mwanaume kushindwa kumpa mwanamke mimba. Kuna mambo mengi yanayowez... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About