Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

ATHARI ZA ULEVI KATIKA JAMII

Featured Image
Watu wanokunywa kupitia kiasi huathiri jamii kwa njia mbalimbali. Madhara mengine hutokea kwa kuwa wanafanya vitu ambavyo wasingevifanya iwapo wasingekuwa wamelewa. Watu wakilewa, huweza kuwa na hasira, wagomvi hivyo basi huwadhuru wengi kiakili na kimwili. Isitoshe, ajali nyingi za kazini na barabarani hutokea watu wakiwa wamelewa. Mara nyingi watu wasiokuwa na hatia na vilema hupoteza maisha yao kutokana na ajali zinazohusiana na ulevi. Watu wanaokunywa pombe kupita kiasi hupunguza uangalifu na hivyo basi kuchangia katika kuenea kwa VVU kwenye jamii. Watu wanaokunywa pombe wanaweza pia kufanya ujambazi katika jamii. Pia wanaokunywa kupita kiasi si wafanyakazi wa kutegemewa kwani hutumia muda mwingi nje ya sehemu zao za kazi. Watu waliozoea kunywa pombe nyingi hupoteza pesa zao nyingi kununua pombe na muda wao mwingi kufikiria jinsi ya kupata pesa za kunywea pombe. Kutokana na gharama za kununua pombe familia zao hukosa pesa za vitu muhimu kama kodi ya nyumba, ada na sare za shule na chakula. Vijana wanaokunywa pombe huanza kuiba pesa nyumbani kwao ili kununulia pombe. Matumizi mabaya ya pombe mara nyingi husababisha matatizo au kuvunjika kwa familia, au urafiki. Vilevile husababisha matokeo mabaya shuleni au kuacha kabisa shule, hali ambayo inaweza kusababisha kukosa nafasi za kazi, kujitegemea wewe mwenyewe na kusaidia famila yako na jamii.
AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Je, kuna madhara gani ya kunywa pombe kwa vijana hasa kijana Albino?

Je, kuna madhara gani ya kunywa pombe kwa vijana hasa kijana Albino?

Athari za pombe kwa mtu anayeishi na ualbino ni sawa na zile
zinazowapata watu wengine.
Read More

Je, ni kweli kwamba uvutaji wa bangi hupunguza mawazo?

Je, ni kweli kwamba uvutaji wa bangi hupunguza mawazo?

Bangi hupunguza mawazo kwa muda mfupi kwani huleta hisia za furaha na utulivu. Lakini hata hivyo ... Read More

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu?

Je, Ni Sahihi Kuanza Kujihusisha na Ngono nikiwa na Mpenzi Wangu? πŸ€”

Jambo zuri kujiuliz... Read More

Haki zinazokiukwa iwapo mvulana au msichana wamelazimishwa kuoa au kuolewa

Haki zinazokiukwa iwapo mvulana au msichana wamelazimishwa kuoa au kuolewa

Nani na lini unaoa ni maamuzi yako binafsi wewe mwenyewe,
hata kama rafiki na wazazi wanakus... Read More

Je, serikali imechukua hatua gani kudhibiti hali hii ya mauaji ya Albino? Tutaishi vipi?

Je, serikali imechukua hatua gani kudhibiti hali hii ya mauaji ya Albino? Tutaishi vipi?

Kifungu cha 14 cha Katiba ya Tanzania kinaeleza kwa ufasaha
kuwa: β€œKila mtu ana haki ya ku... Read More

Vidokezo vya Kutafuta Tarehe ya Muda Mrefu na Msichana

Vidokezo vya Kutafuta Tarehe ya Muda Mrefu na Msichana

Leo hii tutazungumzia kuhusu masuala ya kutafuta tarehe ya muda mrefu na msichana. Inawezekana um... Read More

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aone Thamani Yako

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aone Thamani Yako

Vidokezo vya Kufanya Msichana Aone Thamani Yako

Mara nyingi, kama wanaume, tunataka kuonye... Read More

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Jinsi ya Kuwa na Mawasiliano Mzuri na Msichana

Leo tutazungumzia jinsi ya kuwa na mawasiliano mzuri na msichana. Kwa sababu ya tofauti za kijins... Read More

Je, mvulana atajuaje kama msichana ni bikira? Na pia, msichana anaweza kujitambua vipi kama ni bikira?

Je, mvulana atajuaje kama msichana ni bikira? Na pia, msichana anaweza kujitambua vipi kama ni bikira?

Mvulana hawezi kuthibitisha ubikira wa msichana kwa njia ya kumwangalia wala kwa njia ya kumwingi... Read More

Wakati wa kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume inayopenya kwenye yai, mbegu nyingine zinaenda wapi?

Wakati wa kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume inayopenya kwenye yai, mbegu nyingine zinaenda wapi?

Ni kweli kwamba wakati wa kujamii ana na kutunga mimba ni mbegu moja tu ya kiume i inayopenya kwe... Read More

Mwanamume au mvulana anaweza kubakwa?

Mwanamume au mvulana anaweza kubakwa?

Ndiyo, mtu yoyote anayelazimishwa
kujamiina atakuwa
amebakwa, haijalishi kama
mtu ... Read More

Je, kuna dawa yoyote ya kutibu ugumba?

Je, kuna dawa yoyote ya kutibu ugumba?

Hakuna jibu la ujumla kwa swali hili, kwa sababu tiba ya ugumba inategemea chanzo maalum cha ugum... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About