Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Featured Image

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 3)
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Viazi mbatata (potato 3)
Vitunguu maji (onions 3)
Kitunguu swaum (garlic cloves 4)
Tangawizi iliyosagwa (ginger kiasi)
Hiliki nzima (cardamon 4)
Karafuu (clove 4)
Pilipili mtama (blackpepper 4)
Amdalasini (cirnamon stick 1)
Binzari nyembamba nzima(cumin seeds 1/2 ya kijiko cha chai)
Binzari nyembamba ya kusaga (ground cumin 1 kijiko cha chai)
Chumvi (salt)
Mafuta (vegetable oil)
Nyanya (fresh tomato 3)
Limao (lemon 1)
Pilipili (chilli 1)
Hoho (green pepper)

Matayarisho

Chemsha nyama na chumvi na nusu ya limao mpaka iive kisha weka pembeni. Baada ya hapo andaa vitu vya pilau kwa kuloweka mchele kwenye maji kwa muda wa dakika 10.Menya na kukatakata vitunguu na viazi kisha weka pembeni na pia chemsha maji ya moto na uweke pembeni. Baada ya hapo weka sufuri jikoni na tia mafuta kiasi . Yakisha pata moto tia vitunguu na uvikaange mpaka viwe vya rangi ya kahawia na kisha uitie nyama na ikaange mpaka ipate rangi ya bown pia. Baada ya hapo tia kitunguu swaum na tangawizi na uikoroge vizuri kisha iache ikaangike kwa muda wa dakika 2 kisha tia spice ambazo ni Binzari nyembamba ya unga, hiliki,karafuu, amdalasini na pilipili mtama na viazi. Baada ya hapo unatakiwa ugeuze geuze mpaka mchanganyiko uchanganyike vizuri kisha tia mchele na ugeuzege mpaka uchanganyike na viungo. Baada ya hapo tia chumvi na maji ya kutosha na ukoroge vizuri kisha funika na uache uchemke katika moto wa wastani. Maji yakikaribia kukauka tia binzari nyembamba nzima na ufunike uache mpaka maji yakauke kabisa. maji yakisha kauka ugeuze na ufunike tena na uuache mpaka uive.
Baada ya hapo andaa kachumbali kwa kukatakata vitunguu katika bakuli na kisha tia chumvi kwa ajili ya kuondoa ukali wa vitunguu. Baada ya hapo vioshe mpaka chumvi yote iishe. osha nyanya, Pilipili, hoho na kisha katakata slice nyembamba na uchanganye na vitunguu. Baada ya hapo tia chumvi, kamulia limao na uchanganye zote pamoja. Baada ya hapo chakula kitakuwa tayari kwa kuliwa.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

MAANA YA MANENO YANAYOTUMIKA KATIKA MASUALA YA LISHE

1. Chakula

ni kitu chochote kinacholiwa au kunywewa na kuupatia mwili virutubishi mbalimb... Read More

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Jinsi ya kuandaa Biriani Na Sosi Ya Nyama Ya Mbuzi

Mahitaji

Nyama Ya Mbuzi - 1 Kilo

Mchele - 4 Magi

Vitunguu - 3

Nyanya - ... Read More

Madhara ya soda

Madhara ya soda

Soda ni kiburudisho ambacho si muhimu sana kwa afya.

Aina nyingi za soda zina kafeini ambay... Read More

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Jinsi ya kupika Roast ya biringanya na mayai

Mara nyingi biringanya hutumika kama kiungo cha nyongeza katika mchuzi. Hata hivyo, kiungo hiki k... Read More

Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi

Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi

Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi ๐Ÿฅฆ๐Ÿ‡๐Ÿฅ•๐Ÿฅš๐ŸŒ๐Ÿ’ง๐Ÿฅœ๐Ÿฅ—๐Ÿฅ›๐Ÿ“... Read More

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng'ombe

Viambaupishi Vya Masala

Nyama vipande - 3 LB

Mtindi - ยฝ kopo

Kitunguu (thomu... Read More

Jinsi ya Kupika Kalmati

Jinsi ya Kupika Kalmati

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Hamira (yeast kijiko 1 ... Read More

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Mapishi ya Muhogo Na Mbatata Za Nazi Kwa Nyama Ngombe

Vipimo - Mahitaji Ya Nyama

Nyama ya nโ€™gombe ya mifupa - 3ย lb

Tangawizi mbichi il... Read More

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Mapishi ya Ndizi Mbichi Za Nyama Ng'ombe

Vipimo

Ndizi mbichi - 10

Nyama - kilo 1

Nazi ya kopo - 1

Chumvi - 1 Kij... Read More

Jinsi ya kutengeneza Rock-cakes Za Njugu Na Matunda Makavu

Jinsi ya kutengeneza Rock-cakes Za Njugu Na Matunda Makavu

Mahitaji

Unga - 4 Vikombe

Sukari -10 Ounce

Siagi - 10 Ounce

Mdalasini y... Read More

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ngโ€™ombe Na Mchicha

Mapishi ya wali Wa Nazi Kwa Mchuzi Wa Nyama Ngโ€™ombe Na Mchicha

Wali Wa Mpunga

Mchele wa mpunga - 4 Vikombe

Tui la nazi - 6 vikombe

Chumvi - ... Read More

Jinsi ya kupika Vileja Vya Tambi

Jinsi ya kupika Vileja Vya Tambi

Viambaupishi

Tambi (vermiceli Roasted) Mifuko 2 Siagi 4 Vijiko vya supu Maziwa (condensed... Read More
๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About