Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Jinsi ya kupika Mseto Kwa Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi

Featured Image

Vipimo vya mseto

Tanbihi: Kiasi ya vipimo inategemea wingi wa watu, unaweza kupunguza au kuongeza. Hiki ni kiasi cha watu 6 takriban.

Chooko - 3 Vikombe

Mchele - 2 Vikombe

Samli - 2 vijiko Vya supu

Chumvi - kiasi

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

Safisha na kosha chooko utoe taka taka zote.
Osha mchele kisha roweka pamoja na chooko kwa muda wa saa au zaidi.
Pika chooko na mchele ukiongeza maji inapohitajika, tia chumvi, funika pika moto mdogo mdogo huku unakoroga kwa mwiko kila baada ya muda huku unaponda ponda.
Karibu na kuwiva na kupondeka tia samli endelea kupika hadi karibu na kukauka. Epua.

Samaki

Vipande vya samaki (nguru) - 6 – 7 (4LB)

Kitunguu saumu na tangawizi iliyosagwa - 2 vijiko vya supu

Pilipili ya unga nyekundu - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa ukipenda - 1 kijiko cha chai

Bizari ya samaki - 1 kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Ndimu - kiasi

Mafuta ya kukaangia - kiasi

Namna Ya Kutaysha Na Kupika

Changanya thomu/tangawizi, pilipili, bizari, chumvi pamoja na ndimu iwe masala nzito.
Paka vipande vya nguru kwa masala hayo weka akolee dakika kumi hivi.
Kaanga vipande vya nguru katika mafuta madogo kwenye kikaango (fyring pan) uweke upande.

Mchuzi Wa Nazi

Vitunguu maji – katakata vidogodogo - 4

Nyanya zilizosagwa (crushed) - 3- 4

Nyanya kopo - 1 kijiko cha chai

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Bizari ya mchuzi - 1 kijiko cha chai

Bamia zilizokatwa ndogo ndogo - 2 vikombe

Chumvi - kiasi

Ndimu - 2 vijiko vya supu

Tui la nazi - 3 Vikombe au 800 ml

Namna Ya Kupika

Katika karai au sufuria, tia mafuta ukaange vitunguu hadi vianze kugeuka rangi.
Tia nyanya zilizosagwa, nyanya kopo, uendelee kukaanga, kisha tia bizari, chumvi.
Tia nazi na mwisho tia bamia uache ziwive kidogo tu.
Tia vipande vya samaki vilivyokwisha kaangwa.
Tayari kuliwa na mseto upendavyo.

Vidokezo:

Bizari nzuri kutumia ni ya 'Simba Mbili' inaleta ladha nzuri katika mchuzi.
Ni bora kupika mchuzi kwanza kabla ya mseto kwani mseto ukikaa kwa muda unazidi kukauka.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Boga La Nazi

Mapishi ya Boga La Nazi

Vipimo

Boga la kiasi - nusu yake

Tui zito la nazi 1 Β½ gilasi

Sukari Β½ kikom... Read More

LISHE BORA KWA WATU WENYE AFYA NZURI

LISHE BORA KWA WATU WENYE AFYA NZURI

β€’ Kula chakula bora kunamaanisha kula vyakula aina tofauti ya vyakula kila siku kama vile matun... Read More

Jinsi ya kupika Biriani Ya Nyama Mbuzi Ya Mtindi Na Zaafaraan

Jinsi ya kupika Biriani Ya Nyama Mbuzi Ya Mtindi Na Zaafaraan

Vipimo - Nyama

Nyama mbuzi - 1 kilo

Kitunguu menya katakata - 1

Nyanya/tungul... Read More

Mapishi ya Sambusa za nyama

Mapishi ya Sambusa za nyama

Mahitaji

Nyama ya kusaga (minced beef 1/4 kilo)
Vitunguu maji vilivyokatwakatwa(dice... Read More

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

Mapishi ya Wali Wa Karoti Na Kuku Wa Kukaanga

Vipimo Vya Wali

Mchele wa Basmati/Pishori - 1 kilo moja

Vitunguu maji - 3

Kar... Read More

Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

Jinsi ya kupika Pilau ya Nyama ya Kusaga Na Mboga Mchanganyiko

Mahitaji

Mchele - 2 Mugs

Viazi - 3

Nyama ya Kusaga - 1 Pound

Mboga mcha... Read More

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mapishi ya Mchuzi wa kambale

Mahitaji

Kambale 2
Nazi kopo 1
Nyanya kopo 1
Vitunguu 2
Curry powder ... Read More

Kuandaa Chakula kwa Kupunguza Uzito: Vidokezo na Mapishi

Kuandaa Chakula kwa Kupunguza Uzito: Vidokezo na Mapishi

Kuandaa Chakula kwa Kupunguza Uzito: Vidokezo na Mapishi 🍽️πŸ’ͺ

Kupunguza uzito ni le... Read More

Mapishi ya Biskuti Za Kastadi

Mapishi ya Biskuti Za Kastadi

VIAMBAUPISHI

Unga 6 Vikombe

Sukari ya kusaga 2 vikombe

Siagi 500 gm

Bak... Read More

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mahitaji

Mchele
Kisamvu kilichotwangwa
Samaki
Mbaazi
Nyanya chunguRead More

Upishi wa Afya na Vitoweo vya Hewa: Vinywaji vya Kukoroga na Visivyo na Hatia

Upishi wa Afya na Vitoweo vya Hewa: Vinywaji vya Kukoroga na Visivyo na Hatia

Upishi wa Afya na Vitoweo vya Hewa: Vinywaji vya Kukoroga na Visivyo na Hatia πŸ₯—πŸ₯€

Hak... Read More

Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga

Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga

Mahitaji

Nyama isiyokuwa na mifupa - 1 Β½ Lb(ratili)
Mchele wa Basmati (rowanisha) -... Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About