Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Mapishi ya Biriyani Ya Kuku

Featured Image

Vipimo

Mrowanishe kuku na viungo hivi kwa muda mdogo tu

Kuku (Mkate kate Vipande) - 4 LB

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 2 Vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Pilipili nyekundu ya unga - 1 Kijiko cha supu

Bizari ya manjano (Haldi au Tumeric) - 1 Kijiko cha chai

Bizari ya pilau ya powder (Jeera) - 1 Kijiko cha chai

Gilgilani powder (Dania) - 1 Kijiko cha chai

Ndimu - 1 Kijiko cha supu

Mchele na vitu vya Masala:

Mchele (Basmati mzuri) (rowanisha) - 7 cups

Mafuta ya kupikia - kiasi

Vitunguu Vilivyokatwa - 8

Nyanya iliyokatwa katwa - 3

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi - 1 Kijiko cha supu

Garam Masala -1 Kijiko cha supu

Hiliki powder - Β½ Kijiko cha chai

Tomatoe paste - 1 Kijiko cha supu

Pilipili mbichi zipasue katikati - 4

Chumvi - kiasi

Mtindi - 4 Vijiko vya supu

Kotmiri iliokatwa (Chopped) - Β½ Kikombe

Mafuta ya kunyunyuzia katika wali - 3 Vijiko vya supu

Zaafarani au rangi ya biriani - kiasi

Namna Ya Kutaarisha Na Kupika

Weka kuku aliyerowanishwa na viungo vyake katika Foil tray au chombo chocote utakachomwagia wali humo humo na kupikia biriani, kisha mchome (Bake) mpaka awive na awe mkavu kiasi.

Wakati kuku anapikika, kaanga vitunguu katika karai au sufuria mpaka viwe brown na epua nusu yake weka kando.

Punguza mafuta yabakie kiasi tu, ongeza Thomu na tangawizi, na viungo vyote vya hapo juu isipokuwa Mtindi na kotmiri, endelea kukaanga hadi tomatoe zilainike.

Ongeza chumvi, malizia mwisho kwa kutia mtindi, kotmiri na vile vitunguu ulivyoweka kando. Masala yako tayari.

Mwagia masala juu ya kuku uliyekwishmpika changanya vizuri.

Chemsha Mchele uwive nusu, chuja na mwagia juu ya masala.

Nyunyiza mafuta kidogo juu ya mchele na zaafarani au rangi ya biriani.

Bake katika moto wa 350 – 400 kwa muda wa 15 – 20 minutes. Biriyani imekuwa tayari kuliwa.

Mtindi wa kutolea Biriyani:

Mtindi - 1 kikombe

Pilipili mbichi - 1 ndogo

Kitunguu saumu(/galic) thomu - chembe mbili

Nanaa - kiasi

Chumvi - chembe tu

Weka kwenye Blender na uchanganye, kisha mimina katika bakuli

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Jinsi ya kupika Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

Jinsi ya kupika Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

Viambaupishi

Mchele 3 vikombe

Nyama ya kusaga 1 LB

Mchanganyiko wa Nafaka (up... Read More

Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga

Jinsi ya kupika Biryani ya mbogamboga

Biriani ni miongoni mwa vyakula ambavyo ni nadra sana kupikwa katika familia nyingi tofauti na vy... Read More

Upishi na Matunda ya Mzabibu: Vitamu vyenye Antioxidants

Upishi na Matunda ya Mzabibu: Vitamu vyenye Antioxidants

Upishi na Matunda ya Mzabibu: Vitamu vyenye Antioxidants πŸ‡

Habari za leo wapenzi wa cha... Read More

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

Jinsi ya kutengeneza biskuti za Matunda Makavu Na Cornflakes

VIAMBAUPISHI

Unga - 4 Vikombe

Sukari - 1 Kikombe

Baking powder 1 kijiko cha c... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Ya Keki Kavu kwa kizungu Shortcake

Jinsi ya kupika Biskuti Ya Keki Kavu kwa kizungu Shortcake

Viamba upishi

Unga 2 Magi (vikombe vya chai)

Sukari iliyosagwa 2/3 Magi (kikombe ch... Read More

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende

MAHITAJI

Unga - 4 Vikombe vya chai
Sukari ya laini (icing sugar) - 1 Kikombe cha cha... Read More

Jinsi ya kupika Mitai

Jinsi ya kupika Mitai

VIAMBAUPISHI

Unga wa ngano 1Β 1/2 Kikombe

Baking powder 1 Kijiko cha chai

Bak... Read More

Jinsi ya kupika Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

Jinsi ya kupika Visheti Vyeupe Na Vya Kaukau

VIPIMO:

Unga wa Visheti

Unga 4 Vikombe vya chai

Siagi 1 Kikombe cha chai

<... Read More
Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma (Grilled)

Mapishi ya Biriani Ya Kuku Wa Kuchoma (Grilled)

Mahitaji

Mchele wa Basmati /Pishori - 4 vikombe

Kuku

Vitunguu - 3

Nyany... Read More

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende Na Ufuta

Jinsi ya kupika Biskuti Za Tende Na Ufuta

Viambaupishi

Unga 3 Vikombe vya chai

Baking powder 1 Β½ Vijiko vya chai

Sukar... Read More

Mapishi – Saladi ya Matunda

Mapishi – Saladi ya Matunda

Matunda ni mojawapo wa kundi la vyakula, ni muhimu sana kwa afya bora. Matunda yakitengenezwa viz... Read More

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mapishi ya Wali, samaki wa nazi na kisamvu

Mahitaji

Mchele
Kisamvu kilichotwangwa
Samaki
Mbaazi
Nyanya chunguRead More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About