Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE ๐Ÿ”
โ˜ฐ
AckyShine

Mapishi ya Wali Wa Kukaanga Kwa Nyama Mbuzi Ilichomwa Ya Sosi Ya Ukwaju

Featured Image

Vipimo Vya Wali

Mchele Basmati - 4 vikombe

Vitunguu vya majani (Spring onions) - 5 miche

Pilipili mboga nyekundu (capsicum) - 1

Pilipili mboga manjano (capscimu) - 1

Nyanya kubwa - 1

Supu ya kidonge - 2

Siagi - 2 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele kisha roweka kiasi masaa matatu takriban.
Katakata vitunguu majani, mapilipili boga, nyanya vipande kiasi.
Weka siagi katika sufuria ya kupikia, weka katika moto iyayuke.
Tia vitunguu majani, mapilipili boga, nyanya, kaanga kidogo tu.
Tia mchele kaanga kidogo, kisha tia maji kiasi ya kuivisha mchele.
Tia supu ya kidogo au supu yoyote, funika wali upikike moto. mdogodogo.

Vipimo Vya Nyama Mbuzi Na Sosi Ya Ukwaju

Nyama mbuzi mapande makubwa kiasi - 7/8 vipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi ilosagwa - 1 kijiko cha supu

Ukwaju mzito ulokamuliwa - 1 kikombe cha chai

Jiyra/cummin/bizari pilau - 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo - 2 vijiko vya supu

Siki - 2 vijiko vya supu

Mafuta - ยฝ kikombe cha chai

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Changanya vitu vyote pamoja katika kibakuli kidogo.
Weka nyama katika bakuli kubwa kisha tia mchanganyiko wa sosi, ubakishe sosi kiasi pembeni.
Roweka kwa muda wa masaa 3 โ€“ 5
Panga nyama katika bakuli au treya ya kuchomea katika oven.
Pika (bake) kwa moto wa kiasi kwa muda wa saa takriban.
Karibu na kuiva, epua, zidisha kuichangaya na sosi ilobaki.
Rudisha katika jiko uendelee kuipika muda kidogo tu.
Epua ikiwa tayari, weka juu ya wali uliopakuwa kisha mwagia sosi ya nyanya pilipili (chilii tomato sauce) ukipenda.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mapishi ya bagia na chatney ya machicha ya nazi

Mahitaji

Kunde (Ila mimi nilitumia Nigerian brown beans 1/2 kilo)
Vitunguu maji (oni... Read More

Jinsi ya Kupika skonzi

Jinsi ya Kupika skonzi

Mahitaji

Unga wa ngano (self risen flour 2 vikombe vya chai)
Sukari (sugar 1/2 kijik... Read More

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mapishi ya Pilau ya nyama ya ng'ombe na kachumbari

Mahitaji

Mchele (rice vikombe 3)
Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Viazi mbatata... Read More

Jinsi ya kupika Wali wa hoho

Jinsi ya kupika Wali wa hoho

Wali wa hoho ni chakula maalum kinachotumika katika hafla au sherehe. Ni chakula chenye ladha nzu... Read More

Mapishi ya Biriani la nyama ya ng'ombe

Mapishi ya Biriani la nyama ya ng'ombe

Mahitaji

Nyama ya ng'ombe (beef 1/2 kilo)
Mchele (rice 1/2 kilo)
Vitunguu (onio... Read More

Mambo ya msingi kufahamu kuhusu Lishe

Mambo ya msingi kufahamu kuhusu Lishe

Nini maana ya lishe?

โ€ข Lishe yahusu mafunzo ya chakula na jinsi miili ... Read More

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mapishi ya Haliym Ya Nyama Mbuzi -Bokoboko La Pakistan

Mahitaji

Nyama ya mbuzi au ngโ€™ombe ya mafupa - 2 LB

Mchanganyiko wa dengu (hadesi... Read More

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mapishi ya Biriani Ya Samaki Nguru, Njegere Na Snuwbar (UAE)

Mahitaji

Mchele wa basmati - 4 cups

Samaki nguru (king fish) - 7 vipande au zaidiRead More

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga

Vidokezo 10 vya Vitafunio visivyo na Karanga ๐Ÿฅœ๐Ÿšซ

Kama unapenda kufurahia vitafunio na... Read More

Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo

Jinsi ya kupika mboga ya majani ya mashona nguo

Viamba upishi

Mashonanguo mkono 1
Tui la nazi kikombe 1
Karanga zilizosagwa kik... Read More

Mapishi ya Borhowa

Mapishi ya Borhowa

Mahitaji

Daal (lentils) nyekundu au/na kijani - 1 Kikombe kikubwa

Bizari ya manjano... Read More

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Kamba Wa Nazi, Kisamvu Na Kachumbari Ya Papa Mkavu

Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Kamba Wa Nazi, Kisamvu Na Kachumbari Ya Papa Mkavu

Vipimo - Ugali

Maji - 4 vikombe kiasi inategemea na unga wenyewe.

Unga wa sembe - 2... Read More

๐Ÿ“– Explore More Articles
๐Ÿ  Home ๐Ÿ“– Reading ๐Ÿ–ผ๏ธ Gallery ๐Ÿ’ฌ AI Chat ๐Ÿ“˜ About