Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

Jinsi ya kuandaa Muhogo, Samaki Wa Kuchoma Na Bamia

Featured Image

Mahitaji

Mihongo 3 - 4

Tui - 1000 ml

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu maji kilokatwakatwa - 1

Nyanya mshumaa - 3-4

Pilipili mbichi ndefu - 2-3

Pilipili boga - 2

Namna Ya Kutayrisha Na Kupika

Menya mihogo kisha ikate kate vipande inchi tatu hadi nne, kila kipande kigawe kitoke vipanda vinne. Toa mzizi katikati
Osha mihogo ipange kwenye sufuria ya nafasi na yenye mfiniko, ili upate nafasi ya kutia viungo unavyoona pichani na utokotaji wa tui wahitaji nafasi.
Panga/tandaza kitunguu, nyanya mshumaa/tungule,pilipili mbichi na pilipili boga juu ya mihogo, tia chumvi na tui lote.
Funika sufuria kisha weka jikoni moto wa kiasi kuchemsha tui lipande juu. Hakikisha tui halifuriki na kumwagika kwa kuchungulia au kufunika nusu mfuniko
Kwa mda wa nusu saa hivi ukiona sasa tui linatokota chini chini fuinika mfiniko na upunguze moto mdogo kabisa tui likauke kidogo na liwe zito.
Toa muhogo moja ubonyeze ukiona umewiva zima jiko na wacha sufuria hapo kwa muda wa 10. Mihogo tayari kuliwa.

Kidokezo.

Tui lote huwa chini baada ya mihogo kuwiva unapopakuwa teka kutoka chini uweze kupata uzito wa tui umwagie juu.

Bamia/Mabenda

Bamia - robo kilo

Nyanya - 3

Kitunguu maji - 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au ilosagwa - 1 kijiko cha chai

Nyanya kopo (tomato paste) - 1 kijiko cha supu

Mafuta - 150 ml

Chumvi -1 kijiko cha chai

Pilipili boga - 1

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Kata vichwa vya bamia kisha zikate kate mara mbili zikiwa kubwa, ikiwa ni ndogo mno haina lazima kuzikata osha tu uweke kando.
Katika sufuria, katakata kitunguu, nyanya, pilipili boga tia ndani viungo hivi ongeza chumvi mafuta, thomu na nyanya kop
Washa moto mdogo mdogo huku umefunika sufuria kwa muda wa dakika 20 kisha ukiona mboga zimeshika kutokota ongeza bamia koroga.
Tia maji 200ml wacha kwa muda wa dakika 15 kupikika tena, ukionja utamu wa mboga na chumvi, hakikisha bamia pia zimewiva. Tayari kuliwa.

Samaki Wa Kuchoma

Samaki (dorado) au mikizi au una - 2 wakubwa (fresh)

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu/galic) ya unga au iliyosagwa 1 Β½ cha chai

Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Namna Ya Kutayrisha Na Kuchoma

Safisha samaki vizuri mchane chane (slit) kwa ajili ya kuweka masala.
Changanya viungo vyote na chumvi samaki kisha paka katika samaki kote na ndani ya sehemu ulizochanachana. Mroweke kwa muda wa robo saa hivi.
Weka karatasi ya jalbosi (foil paper) katika treya ya oveni. Muweke samaki kisha mpike (grill) kwa moto wa juu achomeke hadi samaki agueke rangi na awive.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

No comments yet. Be the first to share your thoughts!

Related Posts

Mapishi ya Samaki wa kuokwa

Mapishi ya Samaki wa kuokwa

Mahitaji

Mackerel 2
Kitunguu swaum na tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko c... Read More

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Viambaupishi

  1. Mchele (Basmati) - 3 vikombe
  2. Mbogamboga za barafu (karot, njege... Read More
Mapishi ya mboga ya mnavu

Mapishi ya mboga ya mnavu

Viamba upishi

Mnavu mkono 1
Kitungu 1
Karoti 2
Maziwa kikombe 1
Mafut... Read More

Mapishi ya Ugali, dagaa (wabichi) na matembele

Mapishi ya Ugali, dagaa (wabichi) na matembele

Mahitaji

Dagaa wabichi (Fresh anchovies packet 1)
Unga wa ugali (corn meal flour 1/4... Read More

Mapishi ya Biriani Nyepesi Kupika Ya Samaki

Mapishi ya Biriani Nyepesi Kupika Ya Samaki

Vipimo

Mchele wa pishori (basmati) - 4

Vitunguu katakata - 3

Nyanya (tungule)... Read More

Namna ya kupika Vitumbua

Namna ya kupika Vitumbua

Vitumbua ni aina ya vitafunwa vya chai ambavyo hutengenezwa kwa kutumia unga wa mchele. Kiasili v... Read More

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Afya Ukiwa Safarini

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Afya Ukiwa Safarini

Jinsi ya Kujiandaa kwa Chakula cha Afya Ukiwa Safarini 🍏πŸ₯ͺπŸ›«

Kuwa na lishe bora ni ... Read More

JINSI YA KUANDAA VILEJA

JINSI YA KUANDAA VILEJA

MAHITAJI

Unga wa mchele - 500g

Samli - 250g

Sukari - 250g

Hiliki iliyos... Read More

Jinsi ya kuandaa Wali Wa Hudhurungi Na Kabeji

Jinsi ya kuandaa Wali Wa Hudhurungi Na Kabeji

VIPIMO VYA WALI

Mchele wa hudhurungi (brown rice)

na (wild rice kidogo ukipenda)Osh... Read More

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Viambaupishi

Mchele 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu 1 Mug

(Frozen veg)Read More

Upishi kwa Ajili ya Kusaidia Kinga: Kujenga Uimara

Upishi kwa Ajili ya Kusaidia Kinga: Kujenga Uimara

Upishi kwa Ajili ya Kusaidia Kinga: Kujenga Uimara 🍎πŸ₯¦πŸ‹οΈβ€β™€οΈ

Habari za leo ... Read More

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Jinsi ya kupika Pilau Ya Samaki WaTuna Na Mboga

Viambaupishi

Mchele 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu 1 Mug

(Frozen veg)Read More

πŸ“– Explore More Articles
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About