Warning: Undefined variable $user_id in /home/ackyshine/list.ackyshine.com/sidebar.php on line 36
Sidebar with Floating Button
AckySHINE πŸ”
☰
AckyShine

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Featured Image

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,

Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please log in or register to leave a comment or reply.

Violet Mumo (Guest) on April 20, 2017

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Richard Mulwa (Guest) on April 15, 2017

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Ann Wambui (Guest) on February 2, 2017

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Robert Ndunguru (Guest) on January 26, 2017

Katika imani, yote yanawezekana

David Sokoine (Guest) on November 24, 2016

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Mary Kidata (Guest) on November 4, 2016

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

David Kawawa (Guest) on October 31, 2016

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Alex Nakitare (Guest) on October 29, 2016

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Lydia Wanyama (Guest) on September 14, 2016

Rehema zake hudumu milele

Robert Okello (Guest) on August 25, 2016

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Violet Mumo (Guest) on August 24, 2016

Tumaini ni nanga ya roho

Elizabeth Mrema (Guest) on May 10, 2016

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Alex Nakitare (Guest) on April 7, 2016

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Joyce Mussa (Guest) on March 9, 2016

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Kenneth Murithi (Guest) on January 25, 2016

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Samuel Omondi (Guest) on December 17, 2015

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Mary Mrope (Guest) on November 30, 2015

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

John Lissu (Guest) on November 17, 2015

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Rose Amukowa (Guest) on October 20, 2015

Sifa kwa Bwana!

Lydia Wanyama (Guest) on September 26, 2015

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Joseph Njoroge (Guest) on August 29, 2015

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Alice Wanjiru (Guest) on August 18, 2015

Rehema hushinda hukumu

Simon Kiprono (Guest) on July 25, 2015

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Related Posts

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

AMRI ZA MUNGU

AMRI ZA MUNGU

1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE.
2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO.Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)